1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaAsia

Ujerumani, Ufilipino kuanzisha ushirikiano wa kiusalama

4 Agosti 2024

Ujerumani na Ufilipino zimesema zinafanya kazi ili kufanikisha makubaliano ya ushirikiano katika ulinzi yatakayosainiwa baadaye mwaka huu.

https://p.dw.com/p/4j5c7
Waziri wa Ulinzi wa Shirikisho nchini Ufilipino
Waziri wa Ulinzi wa Ujerumani Boris Pistorius, kushoto, akikutana na mwenzake wa Ufilipino Gilberto Teodoro huko Manila, Ufilipino, Agosti 4, 2024.Picha: Joeal Calupitan/AP/picture alliance

Kauli ya nchi hizo mbili kuhusu ushirikiano wao imetolewa wakati Waziri wa Ulinzi wa Ujerumani Boris Pistorius alipotembelea Manila.

Pistorius na Waziri wa ulinzi wa Ufilipino Gilberto Teodoro, kwa Pamoja wamesema kuwa wanapinga vikali jaribio lolote la upande mmoja  kuendelea na madai ya kujitanua hasa kwa kutumia nguvu au kwa kulazimisha. Hayo yanajiri wakati kukiwa na changamoto za kiusalama barani Asia, Pasifiki na Ulaya.

Makubaliano  hayo ambayo huenda yakawa tayari mwezi Oktoba, yatasaidia kutanua mafunzo kati ya majeshi ya nchi hizo pamoja na ushirikano wa  silaha. Ufilipino imekuwa ikitafuta ushirikiano ili kuimarisha ulinzi wakati kukiwa na mivutano inayoendelea kuongezeka kuhusu Bahari ya Kusini mwa China.