1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mzozo kuhusu makombora ya Taurus Ukraine waendelea Ujerumani

12 Machi 2024

Wanasiasa wa Ujerumani bado wanavutana kuhusu mgogoro uliojitokeza baada ya Urusi kuchapisha mazungumzo ya maafisa wa jeshi la Ujerumani Bundeswehr wakijadili makombora chapa Taurus kwa ajili ya Ukraine.

https://p.dw.com/p/4dQEC
Serikali mjini Kyiv imesema inayahitaji sana makombora hayo kwa ajili ya harakati zake za kuikabili vilivyo Urusi
Serikali mjini Kyiv imesema inayahitaji sana makombora hayo kwa ajili ya harakati zake za kuikabili vilivyo UrusiPicha: Matthias Balk/dpa/picture alliance

Wasiwasi ulishuhudiwa ndani ya muungano unaotawala hapo jana wakati mzozo huo kuhusu kupeleka makombora ya Taurus Ukraine ulipoendelea na kuchochewa kuwa mkubwa na hatua hiyo ya Urusi kuchapisha mazungumzo kati ya maafisa wa jeshi la Ujerumani.

Kansela wa Ujerumani Olaf Scholz amefutilia mbali kupeleka makombora hayo Ukraine angalau kwa sasa, akisema masafa yake ni marefu mno na kwamba Ujerumani huenda ikaburuzwa katika vita vya moja kwa moja iwapo itajaribu kuyapeleka.

Hata hivyo vyama vya upinzani vya Christian Democratic Union CDU na Christian Social Union, CSU, vinaliunga mkono wazo hilo na vinaandaa kura kadhaa bungeni vikipendekeza makombora hayo yapelekwe Ukraine. Kura inayofauta imepangwa kufanyika Alhamisi wiki hii.