1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

KINSHASA: Makundi matatu ya waasi yaweka silaha zao chini

27 Julai 2006
https://p.dw.com/p/CG3Z

Makundi matatu ya waasi katika eneo la mashariki mwa jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo yamekubali kuweka silaha zao chini na kuwaruhusu wapiga kura kushiriki katika uchaguzi utakaofanyika Jumapili ijayo nchini humo.

Msemaji wa kikosi cha kulinda amani cha Umoja wa Mataifa nchini Kongo, Kemal Saiki, amesema mamia ya waasi hao watajumuishwa katika jeshi la taifa kwa kuruhusu uchaguzi ufanyike mkoani Ituri.

Waangalizi wa uchaguzi wa Kongo kutoka Umoja wa Ulaya bado wanaonya kuhusu matatizo ya maandalizi kabla uchaguzi kufanyika.