1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Istanbul yapigwa na tetemeko la ardhi

4 Desemba 2023

Tetemeko la ardhi lenye ukubwa wa 5.1 katika kipimo cha Richter lilipiga eneo la kusini mwa jiji la Istanbul nchini Uturuki siku ya Jumatatu (Disemba 4).

https://p.dw.com/p/4Zki2
Athari za tetemeko la ardhi la mwezi Februari 2023 nchini Uturuki.
Athari za tetemeko la ardhi la mwezi Februari 2023 nchini Uturuki.Picha: ADEM ALTAN/AFP/Getty Images

Kitovu cha tetemeko hilo ni katika ukanda wa pwani wa Gemlik ulio kwenye Bahari ya Marmara umbali wa takriban kilomita 60 kusini mwa Istanbul.

Kulingana na Idara ya Huduma za Dharura ya Uturuki (AFAD, ettemeko hilo halikusababisha uharibifu wowote na pia hakuna mtu aliyejeruhiwa.

Soma zaidi: Idadi ya watu waliokufa kutokana na mitetemeko ya ardhi yapindukia 25,000 nchini Uturuki na Syria.

Kituo cha Utafiti wa Jiologia cha nchini Ujerumani (GFZ) kilisema tetemeko hilo lilikuwa na kasi ya takribani kilomita 10 kwa saa.