1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
Sheria na HakiAfrika

Hali ya utulivu yarudi Nairobi baada ya maandamano

28 Juni 2024

Hali ya utulivu imeanza kurudi katika mji mkuu wa Kenya, Nairobi na maeneo mengine ya nchi hiyo kufuatia maandamano ya jana Alhamisi.

https://p.dw.com/p/4hd1X
Nairobi, Kenya | Hali ya utulivu ikishuhudiwa katika ji wa Nairobi
Askari jeshi ambae analinda doria katika viunga vya mji wa Nairobi kufuatia maandamano ya wananchi.Picha: Daniel Irungu/EPA

Biashara na maduka yamefunguliwa huku wananchi wakiripotiwa kuendelea na shughuli zao za kawaida. 

Maandamano yaliyoongozwa na vijana yalizuka wiki hii baada ya bunge la kitaifa kuupitisha mswada tata wa fedha uliotoa mapendekezo ya kuongeza ushuru kwa mkate na mafuta ya kupikia.

Soma pia:Mahakama Kenya yaidhinisha kutumiwa jeshi kutuliza ghasia

Rais wa Kenya William Ruto alisema hatoutia saini mswada huo wa fedha kufuatia shinikizo la umma.