1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaAsia

China yaihimiza EU kuhusu bahari ya China Kusini

Josephat Charo
2 Septemba 2024

China imeuhimiza Umoja wa Ulaya uwe na haki, umakini na uangalifu na maneno na vitendo kuhusu masuala ya bahari ya China Kusini.

https://p.dw.com/p/4kA9O
Meli ya walinzi wa pwani wa Ufilipino ikiwa imezingirwa na vyombo vya majini vya China katika Bahari ya China Kusini.
Meli ya walinzi wa pwani wa Ufilipino ikiwa imezingirwa na vyombo vya majini vya China katika Bahari ya China Kusini.Picha: Adrian Portugal/REUTERS

Taarifa ya ubalozi wa China katika Umoja wa Ulaya imesema China haijaridhishwa na madai ya Umoja huo dhidi yake kuhusu suala hilo. Taarifa hiyo imesema Umoja wa Ulaya si mdau katika suala la bahari ya China Kusini na haina haki kutoa lawama kuhusu suala hilo.

China na Ufilipino zilituhumiana kwa kugongesha makusudi vyombo vya walinzi wa pwani katika maeneo ya bahari ya China Kusini yanayozozaniwa Jumamosi iliyopita.

Kugongana huko kwa vyombo hivyo karibu na eneo la Sabina ni tukio la tano la malumbano ya baharini katika kipindi cha mwezi mmoja katika uhasama wa muda mrefu kuhusiana na njia hiyo muhimu ya majini.

Umoja wa Ulaya ulisema jana Jumapili kwamba unalaani vitendo hatari vya vyombo vya walinzi wa pwani wa China dhidi ya operesheni halali za Ufilipino katika bahari hiyo.