1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaUkraine

Zelensky amteuwa kamanda mpya wa vikosi vya ardhini

11 Februari 2024

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskiy amemteua Oleksandr Pavliuk, aliyekuwa naibu wa kwanza wa waziri wa ulinzi, kuwa kamanda mpya wa vikosi vya ardhini vya nchi hiyo

https://p.dw.com/p/4cGhV
Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky (kulia) na Oleksandr Pavliuk (katikati) wanaelezwa kuhusu ulinzi wa Ukraine dhidi ya Urusi na luteni jenerali Yurii Sodol (kushoto) mnamo Septzemba 4,2023 katika eneo la Donetsk
Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky (kulia) na Oleksandr Pavliuk (katikati) na luteni jenerali Yurii Sodol (kushoto)Picha: Ukrainian Presidentia/ZUMA/picture alliance

Pavliuk, luteni jenerali aliyehudumu katika wadhifa huo wa wizara kwa muda wa mwaka mmoja, anachukua nafasi ya kanali jenerali Oleksandr Syrskyi baada ya kutimuliwa kwake kuongoza jeshi la Ukraine.

Zelensky atangaza uteuzi wa nyadhifa nyingine za kijeshi

Hapo jana Jumamosi, Rais  Zelenskiy alitangaza uteuzi wa nyadhifa nyingine tano za kijeshi, na kujaza kikosi kinachojiimarisha tena kiulinzi dhidi ya uvamizi wa Urusi nchini humo ambao sasa umedumu kwa takriban miaka miwili.

Soma pia:Urusi yaishambulia tena Kyiv kwa makombora

Ukraine inakabiliwa na uhaba wa wapiganaji na vifaa inapoingia mwaka huu wa 2024 baada ya kupata mafanikio machache katika uwanja wa mapigano mwaka uliopita.

Pia inakabiliwa na hali ngumu kwa kutopokea misaada ya kijeshi kutokaMarekaniambayo ndiyo muungaji wake mkono mkubwa