1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Wanamgambo wawaua zaidi ya raia 45, Ituri

13 Juni 2023

Ujumbe wa ulinzi wa amani huko Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo MONUSCO umesema zaidi ya raia 45 wameuawa baada ya kushambuliwa na wanamgambo katika kambi ya wakimbizi katika jimbo la Ituri, mashairiki mwa taifa hilo.

https://p.dw.com/p/4SVIZ
Watoto wakidandia lori la maji la walinda amani wa Umoja wa Mataifa katika kambi ya wakimbizi wa ndani iliyopo D'jugu, Ituri.
Eneo la mashariki mwa Kongo limekuwa likikabiliwa na mashambulizi yanayofanywa na makundi ya wanamgambo.Picha: Paul Lorgerie/REUTERS

Msemaji wa jeshi katika jimbo la Ituri Jules Ngongo Tshikudi amesema mashambulizi hayo ambayo pia yamesababisha wengine 10 kujeruhiwa kuwa ni "kitendo cha hujuma" dhidi ya majaribio ya kurejesha amani na kusema uchunguzi unaendelea.

Taarifa ya MONUSCO imelitaja kundi la waasi wa CODECO, ambalo limetapakaa katika eneo hilo tete la mashariki kuwa linahusika na mauwaji hayo katika kambi iitwayo "LALA".

CODECO ni kundi ambalo linajinasibu kulinda maslahi ya jamii ya wakulima ya Lendu. Kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa wapiganaji wake wamewaua mamia ya raia katika eno la Ituri na kuwalizimisha maelfu ya watu kuyakimbia makazi yao.