1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

UTALII BERLIN (ITB)

11 Machi 2005
https://p.dw.com/p/CFXv

BERLIN:

Waziri wa misaada ya maendeleo wa Ujerumani,Bibi Heidemarie Wiecorek-Zeul amewataka hii leo watalii kurejea kutembelea maeneo yaliokumbwa na maafa ya Tsunami .Akizungumza kabla ya ufunguzi rasmi wa Maonesho ya mwaka huu ya kimataifa ya utalii mjini Berlin (ITB), waziri huyo alisema utalii ndio unaotoa msaada bora kabisa kwa nchi za kusini-mashariki mwa Asia zilizoathirika na mawimbi hayo makubwa ya Tsunami.