Urusi inajaribu kuonesha hali ni shwari baada ya uasi wa kundi la mamaluki la wagner. Kitisho hicho cha uasi kilidumu kwa saa kadhaa siku ya Jumamosi kiliongozwa na kiongozi wa kundi hilo Yevgeny Prigozhin. Tukio hilo linadaiwa kuyumbisha udhibiti wa madaraka wa rais wa Urusi Vladimir Putin.