1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroSudan

UN yasema eneo la Darfur Kusini lapokea msaada wa chakula

20 Juni 2024

Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) limesema eneo la kusini mwa Darfur linahitaji msaada zaidi wa kiutu, licha ya eneo hilo kushuhudia ongezeko kidogo la misaada muhimu inayoingia.

https://p.dw.com/p/4hJsK
Mgogoro wa njaa Sudan
WFP inasema zaidi ya watu 50,000 wanakabiliwa na njaa kote Darfur KusiniPicha: AFP

Ujumbe wa WFP nchini Sudan umesema zaidi ya watu 50,000 wanakabiliwa na njaa kote Darfur Kusinihuku WFP ikijitahidi kuwafikishia msaada wa chakula kwa ushirikiano na shirika la misaada la World Vision.

WFP imesema sehemu nyingi za nchini Sudan, zimetumbukia kwenye mgogoro tangu mwezi April mwaka jana, yalipozuka mapigano makali kati ya jeshi la Sudan na kikosi cha wanamgambo cha RSF.

Soma pia: UN yaonya uwezekano wa janga la kibinadamu al Fashir

Mkuu wa masuala ya wakimbizi wa Umoja wa Mataifa Filippo Grandi, aliyehitimisha jana Jumatano ziara yake ya pili nchini Sudan tangu vita vilipoanza, ametahadharisha kwamba nchi hiyo inakaribia kutumbukia kwenye baa la njaa.

Naibu msemaji wa Umoja wa Mataifa Farhan Haq, amesema mvua kubwa zinazozotarajiwa hivi karibuni zinaweza kusababisha mafuriko makubwa ambayo yatazuia shughuli za kufikisha misaada.