1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

UN: Karibu watu milioni moja wameyahama makazi yao DRC

8 Oktoba 2024

Takriban watu milioni moja wameyakimbia makazi yao mwaka huu nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

https://p.dw.com/p/4lXim
Kambi ya IDP ya Rusayo huko Mashariki ya Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
Picha hii, iliyopigwa Oktoba 2, 2023, inaonyesha kambi ya Rusayo, makao ya maelfu ya watu waliokimbia makazi yao kutokana na vita, viungani mwa Goma Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.Picha: Alexis Huguet/AFP

Hayo ni kwa mujibu wa mkuu wa masuala ya haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa.Volker Turk amesema ukiukwaji wa haki za binaadamu unaongezeka na kwamba hali nchini Kongo inazidi kuwa mbaya kila uchao, huku akitaja wasiwasi wake kutokana na kuongezeka kwa idadi ya watu wanaosubiri kunyongwa baada ya DRC kurejesha hukumu ya kifo.Turk, ambaye aliitembelea DRC mwezi April, ameliambia Baraza la Haki za Kibinadamu la Umoja wa Mataifa kwamba nchi hiyo ya Afrika ya kati inakabiliwa na ongezeko kubwa la ghasia, kuhatarisha maslahi ya kikanda na kimataifa, unyonyaji wa mashirika kadhaa na utawala dhaifu wa sheria.