1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
Sheria na HakiAfrika

MSF: Wakimbizi wa ndani Kongo wakabiliwa na ukatili

6 Agosti 2024

Utafiti kutoka shirika la hisani la kimataifa la madaktari wasio na mipaka MSF imesema ukatili, hasa wa kingono unafanywa kila siku ndani na karibu na kambi za wakimbizi wa ndani mashariki ya Kidemokrasia ya Kongo.

https://p.dw.com/p/4jBEx
Muhudumu wa afya MSF akimuhudumia mgonjwa
Muhudumu wa afya MSF akimuhudumia mgonjwa.Picha: MSF/AP Photo/picture alliance

 Ripoti kutoka kundi la Epicentre, linalohudumu chini ya MSF, ambayo ilifanya uchunguzi katika kaya zinazoishi katika kambi nne magharibi mwa Goma, imesema zaidi ya mmoja kati ya wanawake 10 waliripoti kubakwa kati ya Novemba 2023 hadi Aprili 2024. 

Taarifa ya MSF imesema kuwa kwa mara nyingine, waathiriwa wa unyanyasaji wa kingono wanaripoti kushambuliwa na wanaume, aghalabu wenye silaha, katika misitu na viwanja ambako wanapaswa kwenda kutafuta kuni au chakula wanachohitaji kuzilisha familia zao.

Camille Niel, mratibu wa masuala ya dharura wa MSF mjini Goma amesema hali yao tete, pamoja na makazi duni ya muda wanaoishi, vinafanya kuwa katika mazingira hatari ya aina hii ya ukatili.

Kundi la waasi wa M23, ambalo lilikuwa limetulia kwa karibu muongo mmoja, lilianzisha mashambulizi katika mkoa wa Kivu Kaskazini, na kuwauwa watu kadhaa huku mamia kwa maelfu ya wengine wakiyakimbia makazi yao.