1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ujerumani yafungua Sinagogi jipya Magdeburg

10 Desemba 2023

Sinagogi jipya limefunguliwa hii leo katika mji wa Magdeburg, Mashariki mwa Ujerumani, miaka 85 baada ya kuharibiwa katika mashambulizi dhidi ya wayahudi ya mwaka 1938.

https://p.dw.com/p/4ZzVA
Ujerumani I Sinagogi jipya Magdeburg
Ufunguzi wa Sinagogi jipya MagdeburgPicha: Klaus-Dietmar Gabbert/dpa/picture alliance

Waziri Mkuu wa jimbo la Sachsen-Anhalt Reiner Haseloff amesema sinagogi hilo jipya linasimamia masuala ya kuishi kwa pamoja kwa amani.

Ameongeza kuwa maisha ya wayahudi katika jimbo hilo yanathaminiwa na kutambuliwa. Kwa upande wake kiongozi wa Baraza la wayahudi Josef Schuster, amesisitiza kuwa leo ni siku ya furaha na ya kujivunia.

Soma zaidi: Scholz asikitishwa na kuenea visa vya chuki kwa Wayahudi

Jengo hilo jipya limegharimu dola milioni 8.1 na lilijengwa kwa hisani ya juhudi za raia wa jimbo hilo waliokusanya michango ya kujenga eneo jipya la kuabudu. Jimbo la Saxony-Anhalt liligharamia sehemu kubwa ya ujenzi wa sinagogi hilo.