1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ujerumani na Zanzibar zarejesha rasmi uhusiano

Salma Said26 Januari 2022

Serikali ya Zanzibar na Ujerumani leo Jumatano Januari 26,2022 zimetangaza rasmi kurejesha uhusiano uliovunjika baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.

https://p.dw.com/p/466M9
Sansibar | Gemeinsamer Workshop zwischen der Regierung von Sansibar und der Bundesrepublik Deutschland
Picha: Salma Said/DW

Katika sherehe zilizofanyika leo, kuitangazia dunia kurudishwa uhusiano huo, Rais wa Zanzibar Daktari Hussein Ali Mwinyi amesema ni wakati mzuri ambapo Zanzibar itanufaika katika maeneo mengi ya maendeleo hasa Afya, upatikanaji wa maji na michezo kwa miaka mitano ijayo ambapo msaada ya kuimarisha michezo ni muhimu kwa maendeleo ya Zanzibar.

Rais amesema huduma za afya bado ni changamoyo na serikaili ya Ujerumani itasaidia kuanzisha bima ya afya ili wananchi wasaidiye kuchangia bajeti ya afya, tatizo la maji bado ni kubwa na serikali imekubali kuangalia kwa undani sababu za ukoesefu wa maji Zanzibar.

''Kwamba watatusaidia ( Ujerumani) katika sekta tatu kubwa,ya kwanza ni afya, ya pili ni maji na ya tatu ni mechezo. Katika afya wakotayari kutusaidia katika suala zima la kuanzisha huduma ya bima za afya kwa wote.'',alisema Mwinyi.

Soma pia :Zanzibar yawavutia wawekezaji

''Tuna maadili yanayofanana''

Balozi wa Ujerumani nchini Tanzania,Regine Hess amesema nchi yake na Zanzibar  zinamaadili yanayofanana
Balozi wa Ujerumani nchini Tanzania,REgine Hess amesema nchi yake na Zanzibar zinamaadili yanayofananaPicha: Salma Said/DW

Akizungumza katika uzinduzi huo wa balozi wa ujerumani nchini Tanzania Bi Regine Hess alisema sera ya ujerumani na nchi za jumuia ya ulaya (EU) ni kuheshimu haki za binadamu na demokrasia na kwanza Zanzibar imeanza vizuri ndio maana ujerumani umeamuwa kurejesha uhusiano na Zanzibar.

Uhusiano mpya wa Zanzibar na ujerumaini utasimamiwa na kutekelezwa na taasisi za GITZ na banki ya KFW ambapo wawakilishi wa taasisi hizo walisema majadilianoya kurudisha mahusiano huo umefanyika siku mbili zilizopita katika maeneo waliyokubaliana.

Soma pia :Wazanzibari wahimizwa kudumisha amani

Uhusiano kati ya Ujerumani na Zanzibar ulianza mwaka 1965 katika maneno mbali mbali ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa nyumba, na kuimarishwa huduma za kijamii.