1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ukraine itashinda vita iwapo itaendelea kupata msaada

30 Mei 2024

Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kujihami ya NATO, Jens Stoltenberg amesema Ukraine inaweza kupata mafanikio katika vita dhidi ya Urusi lakini linategemea uungaji mkono usioyumba kutoka washirika wa mfungamano huo wa kijeshi.

https://p.dw.com/p/4gT2H
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kujihami ya NATO, Jens Stoltenberg
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kujihami ya NATO, Jens StoltenbergPicha: Efrem Lukatsky/AP Photo/picture alliance

Stoltenberg ametoa matamshi hayo muda mfupi kabla ya kuanza kwa mkutano wa mawaziri wa mambo ya kigeni wa nchi wanachama wa NATO nchini Jamhuri ya Czech. 

Mkutano huo kwa sehemu kubwa utatawaliwa na suala la mzozo wa Ukraine hususani shinikizo linaloongezeka la kuyataka mataifa ya magharibi kutoa ruhusa kwa nchi hiyo kutumia silaha inazopokea kushambulia ndani ya Urusi.

Soma pia:Mawaziri wa kigeni wa NATO wanafanya mkutano Jamhuri ya Czech

Akizungumza mjini Prague, Stoltenberg amegusia suala hilo akisema ni wakati kwa washirika wa Ukraine kutafakari upya vizuizi vilivyopo kwa sababu vinahujumu uwezo wa nchi hiyo kujilinda dhidi ya Urusi.