1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaSenegal

Sonko aahidi kusaidia kambi yake kushinda uchaguzi

16 Machi 2024

Kiongozi wa upinzani nchini Senegal Ousmane Sonko ameapa jana Ijumaa kusaidia kambi yake kushinda uchaguzi wa urais wa Machi 24 licha ya kuzuiwa kupiga kura.

https://p.dw.com/p/4dnIB
Kiongozi wa upinzani nchini Senegal Ousmane Sonko aahidi kupambania ushindi wa urais
Mpinzani mkubwa wa serikali ya Senegal Ousmane Sonko, alipokuwa akizungumza wakati wa maandamano ya upinzani katika eneo la Place de l'Obelisque huko Dakar, Juni 8, 2022.Picha: Seyllou/AFP

Sonko amesema hayo katika hotuba yake ya kwanza hadharani kenye mkutano wa kampeni tangu alipoachiliwa kutoka gerezani siku ya Alhamisi, baada ya kuzuiwa kwa miezi kadhaa gerezani.

Kwenye hotuba hiyo fupi, Sonko alirudia kutaja baadhi ya ahadi zake muhimu alizozitoa wakati wa kampeni ambazo ni pamoja na umuhimu wa kupambana na rushwa serikalini na kulinda uchumi wa Senegal katikati ya ushawishi wa mataifa ya kigeni.

Mshirika wake mkuu, Bassirou Diomaye Faye, ambaye pia aliachiliwa kutoka gerezani, atagombea nafasi hiyo ya urais.

Kuachiliwa kwao kunafuatia amri ya Rais Macky Sall ya kuwafutia hatia za kisiasa wafungwa, ikiwa ni pamoja na mamia waliokamatwa katika maandamano ya mwisho mwaka.

Maandamano yamelikumba taifa hilo kwa mara nyingine na kutikisa sura ya Senegal ambayo ni nguzo ya utulivu katika eneo la Afrika Magharibi. Tangu kupata uhuru kutoka Ufaransa katika 1960, imefanya uchaguzi wa mara kwa mara na haijawahi kufanya mapinduzi, tofauti na mataifa mengine mengi katika eneo la Sahel.

Kufuatia kuachiliwa kwa Sonko Alhamisi usiku, Dakar alifurika maelfu ya watuwaliokuwa wakiimba na kucheza huku kukishuhudiwa misafara ya wafuasi wake.