1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rais wa Iran aanza ziara China,makubaliano kadhaa kuafikiwa

14 Februari 2023

Rais wa Iran Ebrahim Raisi amewasili China leo kwa ziara ya siku tatu, akiambatana na ujumbe mkubwa unaomjumuisha gavana wake wa benki kuu na mawaziri wa biashara, uchumi na mafuta.

https://p.dw.com/p/4NSAl
Iran, Teheran | 44. Jahrestag der Islamischen Revolution
Picha: Iranian Presidency/ZUMA/picture alliance

Raisi atafanya mazungumzo na mwenzake wa China, Xi Jinpingkatika mji mkuu Beijing, ambapo wawili hao wanatarajiwa kusaini nyaraka kadhaa za ushirikiano. 

Iran na China zina uhusiano imara wa kiuchumi, hasa katika nyanja za nishati, usafiri, kilimo, biashara na uwekezaji, na mwaka 2021 zilisaini mkataba wa miaka 25 wa ushirikiano wa kimkakati.

Soma pia:Rais wa Iran kufanya ziara nchini China

Mataifa hayo yote mawili yanakabiliwa na shinikizo kutoka Marekani kuhusiana na misimamo yao kuhusu uvamizi wa Urusi nchini Ukraine, huku Iran ikiwa imewekewa vikwazo na Marekani kutokana na mpango wake wa nyuklia.