1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
Migogoro

NATO iliyotanuliwa yaanza luteka Finland, Norway na Sweden

4 Machi 2024

Vikosi vya jumuiya ya kijeshi ya NATO leo vimeanza luteka za kijeshi juu ya kulilinda eneo lake jipya la Ulaya kaskazini.

https://p.dw.com/p/4d9wa
Bendera za Finland
Finland imejiunga hivi karibuni na jumuiya ya NATOPicha: picture alliance/Zoonar

Zaidi ya wanajeshi 20,000 kutoka mataifa 13 wanashiriki katika mazoezi hayo yatakayochukua karibu wiki mbili kwenye maeneo ya kaskazini ya Finland, Norway na Sweden.

Wizara ya ulinzi ya Finland, ambayo ni mwanachama mpya wa NATO, imesema wanajeshi wake zaidi ya 4,000 wanashiriki kwa mara ya kwanza katika operesheni ya ulinzi wa pamoja wa kikanda kwenye muungano huo.

Soma pia: Mazoezi makubwa ya kijeshi ya NATO yaanza Norway

Finland iliyo na mpaka wa kilomita 1,340 kati yake na Urusi, ilijiunga na NATO mnamo mwezi uliopita. Nchi jirani yake ya Sweden kwa sasa imo kwenye mchakato wa kukamilisha taratibu za kuingia katika muungano wa kijeshi wa NATO kama mwanachama wake wa 32.