Unakaribia mwezi mmoja tangu kulipozuka vita vya Israel dhidi ya kundi la Hamas katika Ukanda wa Gaza baada ya shambulizi la kushutukiza la wanamgambo wa Hamas. Mashirika ya Umoja wa Mataifa yametoa tamko la pamoja la usitishaji mara moja wa machafuko hayo. Wapalestina takribani 10,000 wameuawa kwa mujibu wa wizara ya afya inayosimamiwa na kundi la Hamas. #kurunzi