1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mpango usitishwaji mapigano kati ya Israel-Hamas watekelezwa

24 Novemba 2023

Mpango wa kusitisha mapigano kwa muda wa siku nne kati ya Israel na kundi la Hamas umeanza kutekelezwa leo asubuhi.

https://p.dw.com/p/4ZOh1
Wanajeshi wa Israel wakilinda doria karibu na hospitali ya Al Shifa
Wanajeshi wa Israel wakilinda doria karibu na hospitali ya Al ShifaPicha: Ronen Zvulun/Reuters

Kundi la kwanza la mateka 13 ambao ni wanawake na watoto wanaoshikiliwa na Hamas wanatarajiwa kuachiwa huru baadae leo, huku Israel nayo ikiwaachia wafungwa Wakipalestina wapatao 150.

Malori ya mafuta yamefanikiwa pia kuingia Gaza kupitia kivuko cha mpakani cha Rafah.

Awali, Misri ilisema lita 130,000 za dizeli, lori nne za gesi na malori 400 ya misaada ingelisafirishwa kila siku hadi Gaza.

Soma pia:Usitishwaji mapigano kuanza Gaza, mateka kuachiwa

Makubaliano hayo yanaleta ahueni kwa wakaazi milioni 2.4 wa Gaza ambao wamekuwa wakikabiliwa na wiki saba za mashambulizi ya kulipiza kisasi ya Israel baada ya shambulizi la Hamasla Oktoba 7 ambalo Israel inasema watu 1,200 waliuawa.

Nayo mamlaka ya Hamas, imesema hadi sasa tayari watu 15,000 wameuawa.