1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mgombea wa upinzani Uganda alalamikia unyanyasaji wa polisi

Admin.WagnerD2 Desemba 2020

Mgombea urais nchini Uganda Robert Kyagulanyi ameshinda katika makao makuu ya tume ya uchaguzi kwa ajili ya kuwasilisha lawama za namna wanavyohujumiwa na kunyanyaswa na vyombo vya usalama.

https://p.dw.com/p/3m81T
Uganda Festnahme Robert Kyagulanyi aka Bobi Wine
Picha: Abubaker Lubowa/REUTERS

Mgombea huyo maarufu kama Bobi Wine alisitisha kampeni zake hapo jana wakati walinzi wake wawili walipojeruhiwa na kile kinachodaiwa kuwa vilipuzi walivyotupiwa na polisi. Hata hivyo polisi imekanusha madai hayo ikisema kuwa kuna baadhi ya raia walio na vilipuzi kama hivyo.

Hali ilikuwa ya taharuki tangu asubuhi kwenye makao makuu ya tume ya uchaguzi pamoja na yale ya chama cha NUP wafuasi wa chama hicho wakisubiri matokeo ya mashauriano kati ya viongozi wao na wakuu wa tume ya uchaguzi. Viongozi wa NUP wakiongozwa na Bobi Wine waliwasilisha ushahidi kuhusu mienendo ya vyombo vya usalama kwa kuwahangaisha kila wanakokwenda kuendesha kampeni zao kwa mujibu wa ratiba na sheria walizopewa na tume hiyo. Waandishi wa habari hawakuruhusiwa katika kikao hicho lakini ulipokamilika.

Mgombea Bobi Wine asitisha kampeni zake nchini Uganda

Uganda Kampala | Porträt von Robert Kyagulanyi, Präsidentschaftskandidat
Bango la picha ya mgombea Bobi WinePicha: Lubega Emmanuel/DW

Hapo jana Bobi Wine alisitisha kampeni zake  baada ya walinzi wake wawili na wafuasi kadhaa kujeruhiwa mjini Jinja. Ameitaka tume ya uchaguzi ihakikishe kuwa vyombo vya usalama vinaheshimu haki yake kutafuta kura. Huku baadhi ya wafuasi wa chama chake wakipendekeza uchaguzi uahirishwe kwani mazingira ya sasa si salama kwa zoezi huru na la amani la kidemokrasia.

Kwa upande wao polisi wanasisitiza kuwa wanafuata sheria na kanuni zilizowekwa katika kuendesha kampeni na hawaonekani kukubali lawama zozote wanazotupiwa. Huku kampeni hizo za urais zikingia wiki ya nne, angalau wagombea wote dhidi ya rais Museveni wamejikuta wakikabiliana na vyombo vya usalama pale wanapozuiliwa kuwafikia wananchi kuwaelezea sera zao lakini  Bobi Wine ndiye ambaye ameonekana kuandamwa zaidi anasema. 

Soma zaidi:Museveni na Bobi Wine walaumiana kuhusu vifo vya raia

Kwa upande wake, rais Museveni ameendesha kampeni zake akikutana tu na viongozi wa wilaya na kanda. 

Chanzo: DW