1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaYemen

Marekani: Vikosi vya Iran na Hezbollah vinawasaidia Wahouthi

28 Februari 2024

Marekani imesema vikosi kutoka Iran na mshirika wake wa Lebanon, kundi la Hezbollah, vinafanya kazi ndani ya Yemen kuwasaidia waasi wa Kihouthi kufanya mashambulizi dhidi ya meli za kimataifa.

https://p.dw.com/p/4cxiW
Mmoja wa wapiganaji wa kundi la Wahouthi nchini Yemen
Mmoja wa wapiganaji wa kundi la Wahouthi nchini YemenPicha: Mohammed Hamoud/Anadolu/picture alliance

Mjumbe maalum wa Marekani kwa Yemen Tim Lenderking ameiambia kamati ndogo ya baraza la Seneti la Marekani kwamba serikali ya Iran inatoa vifaa na kupiga jeki mashambulizi yanayofanywa na waasi wa Houthi. 

Mnamo mwezi Disemba, Ikulu ya White House ilisema kuwa Iran inahusika na kupanga mashambulizi dhidi ya meli za kimataifa katika bahari ya Sham.

Soma pia: Wahouthi washambulia meli nje ya pwani ya Kusini mwa Yemen 

Kundi la Wahouthi limeeleza kuwa linafanya mashambulizi hayo kama ishara ya kuonyesha mshikamano na Wapalestina.

Mashambulizi hayo ya Wahouthi yamekuwa na athari kubwa kwa biashara ya kimataifa na kulazimisha baadhi ya kampuni za meli kubadilisha njia na kuzunguka kusini mwa Afrika ili kuiepuka bahari ya Sham.

Wiki iliyopita, Misri ilisema mapato katika mfereji wa Suez yalipungua kwa hadi asilimia 50 mwaka huu.