1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Machafuko yaendelea Senegal yakishinikiza uchaguzi

14 Februari 2024

Mamlaka ya Senegal inakabiliwa na hasira zinazoongezeka za raia na shinikizo kutoka kwa jamii ya kimataifa baada ya serikali kuzima mawasiliano ya simu na kupiga marufuku maandamano ya kupinga kuahirishwa uchaguzi..

https://p.dw.com/p/4cP1w
Senegal Dakar | Wafuasi wa vyama vya upinzani wanaoshinikiza uchaguzi
Wafuasi wa vyama vya upinzani wanaoshinikiza uchaguzi wa rais kufanyika wakitawanywa kwa mabomu ya machoziPicha: Stefan Kleinowitz/AP/picture alliance

Hatua ya Rais Macky Sall ya kuahirisha uchaguzi uliopangwa kufanyika Februari 25 hadi mwezi Disemba, imeitumbukiza Senegal kwenye mgogoro mbaya.  

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ameuambia utawala wa Senegal kuwa ni muhimu na ni haki ya Wasenegal wote kuheshimiwa pale wanapokusanyika kueleza hisia zao kwa amani.

Soma pia:Uchumi wa Senegal kuzorota kutokana na mkwamo wa kisiasa

Msemaji wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Stephane Dujarric amesema Guterres ametoa wito wa kutatuliwa mgogoro wa Senegal kwa njia zilizowekwa za kikatiba.

Ufaransa ambayo ni mkoloni wa zamani wa taifa hilo la Afrika Magharibi ameitaka Senegal ihakikishe inatoa majibu sahihi kuhusiana na maandamano na imetaka kura ya rais ifanyike haraka iwezekanavyo.