1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

IMF yaidhinisha mkopo wa dola milioni 786 kwa Tanzania

21 Juni 2024

Shirika la Fedha Duniani (IMF) limeidhinisha mpango mpya wa mkopo wenye thamani ya karibu dola milioni 786 kwa Tanzania, ili kuisaidia kujenga uwezo wa kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi.

https://p.dw.com/p/4hLpJ
Samia Suluhu Hassan
Rais Samia Suluhu Hassan wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.Picha: Presidential Press Service Tanzania

Bodi ya IMF imeipatia Tanzania fedha nyengine karibu dola milioni 150, baada ya kuafiki kuwa nchi hiyo imekamilisha vigezo muhimu chini ya mpango wa awali wenye thamani ya zaidi ya dola bilioni moja, ulioongezewa muda wa miezi sita zaidi hadi Mei mwaka 2026.

Soma zaidi:Zambia yaagizia maelfu ya tani za mahindi kutoka Tanzania 

Naibu Mkurugenzi Mkuu wa IMF, Bo Li, ameusifu utendaji wa Tanzania pamoja na ajenda yake ya mageuzi.

Kulingana na shirika hilo la fedha duniani, ukuaji wa uchumi wa Tanzania uliongezeka mwaka jana huku mfumuko wa bei ukidhibitiwa.