1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaIsrael

Hamas yaapa kujibu mashambulizi ya Israel Ukanda wa Gaza

28 Oktoba 2023

Kundi la Hamas limeapa kuwa tayari kujibu kwa "nguvu isiyo mfano" mashambulizi ya Israel baada ya jeshi la nchi hiyo kutangaza kutanua kampeni yake ya kijeshi kwenye Ukanda wa Gaza ikijumuisha operesheni ya ardhini.

https://p.dw.com/p/4Y8wd
Kifaru cha Israel kikiwa karibu na mpaka wa Ukanda wa Gaza
Kifaru cha Israeli kikipiga doria kwenye mji wa kusini mwa Israel wa Sderot jirani na mpaka na GazaPicha: Aris Messinis/AFP/Getty Images

Kundi hilo la wanamgambo wa Kipalestina linalotawala Ukanda wa Gaza limearifu kwamba wapiganaji wake tayari wanakabiliana na vikosi vya Israel kwenye maeneo ya mpaka, kufuatia tangazo la Israel kuwa litazidisha mashambulizi yake ndani ya Gaza.

Kulingana na wizara ya afya ya Gaza, mashambulizi hayo ya Israel yamewauwa zaidi ya watu 7,000 kwenye ukanda huo tangu yalipoanza mwanzoni mwa mwezi huu kujibu shambulizi baya kabisa la kundi la Hamas la mnamo Oktoba 7.

Siku hiyo wanamgambo wa Hamas waliingia Israel na kufanya mauaji ya watu 1,400 na kuwachukua mateka mamia wengine. Israel, Marekani na mataifa mengine kadhaa ya magharibi yameliorodhesha kundi la Hamas kuwa la kigaidi.