1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaMarekani

Haley aapa kutojiengua iwapo atashindwa kura za mchujo

24 Januari 2024

Mpinzani mkuu wa mwisho wa Donald Trump anayewania nafasi ya kupeperusha bendera ya chama cha Republican, Nikki Haley, amesema hatojiengua hata iwapo atashindwa kwenye kura za mchujo katika jimbo la New Hampshire.

https://p.dw.com/p/4bbgL
Marekani | Jimbo la Iowa | Nikki Haley
Mpinzani mkuu wa Donald Trump anayewania nafasi ya kupeperusha bendera ya chama cha Republican katika uchaguzi wa mwezi Novemba Nikki HaleyPicha: Cody Scanlan/The Des Moines Register/AP/picture alliance

Washirika wa Donald Trump wamemuwekea shinikizo balozi huyo wa zamani wa Marekani katika Umoja wa Mataifa kujiondoa kwenye kinyang'anyiro hicho iwapo atashindwa kwa kura nyingi.

Haley amewekeza raslimali nyingi katika jimbo hilo akitaraji kupata uungwaji mkono hasa miongoni mwa wanaompinga Trump na kushinda kura hizo za mchujo au angalau kupoteza kwa kura kidogo.

Kwa mujibu wa kura ya maoni iliyofanywa na shirika la habari la AP, wafuasi wengi wa Republican wana mashaka juu ya ushindi wa Trump katika jimbo la New Hampshire tofauti kabisa na Iowa, ambapo rais huyo wa zamani alipata ushindi katika kura za mchujo zilizofanyika wiki iliyopita.