1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ghasia zazuka katika kambi ya wakimbizi ya Kakuma nchini Kenya

8 Mei 2008

Nchini kenya ghasia zinaripotiwa kutokea katika kambi ya wakimbizi ya Kakuma iliyo kaskazini mwa nchi.

https://p.dw.com/p/DwoL

Watu kadhaa wanaripotiwa kujeruhiwa na mkaazi mmoja kupigwa risasi hadi kufa wakati wa mapigano hayo.Kambi hiyo ilianzishwa mwaka 92.Yapata wakimbizi elfu 70 wanapata hifadhi katika kambi hiyo wengi wao kutoka nchi za Somalia,Sudan ,Ethiopia na hata Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo.

Ili kupata picha halisi Thelma Mwadzaya alizungumza na John mkimbizi kutoka Kongo anayepata hifadhi katika kambi hiyo.