1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

EU: Yaweka vikwazo kwa utawala wa kijeshi Niger

23 Oktoba 2023

Umoja wa Ulaya hii leo umechukua hatua ya kisheria ya kuuweka vikwazo utawala wa kijeshi wa Niger uliochukua madaraka katika mapinduzi ya mwezi Julai.

https://p.dw.com/p/4Xv2m
Mkuu wa Sera za Kigeni wa Umoja wa Ulaya Joseph Borrell
Mkuu wa Sera za Kigeni wa Umoja wa Ulaya Joseph BorrellPicha: FREDERICK FLORIN/AFP

Umoja huo wenye wanachama 27 aidha umeilaani hatua ya kumuondoa rais aliyechaguliwa kidemokrasia, Mohamed Bazoum, ambaye ni mshirika mkubwa wa mataifa ya Magharibi.

Umoja wa Ulaya umetangaza kupitisha mfumo wa kisheria ambao utauwezesha kuwawekea vikwazo watu binafsi na vyombo vinavyohusika na vitendo vinavyotishia amani, utulivu na usalama wa Niger.

Soma pia:Kiongozi wa zamani wa Niger pamoja na familia yake wanaendelea vizuri

Mkuu wa sera za kigeni wa Umoja huo, Joseph Borrell, amesema hatua hiyo inatuma ujumbe wa wazi kwamba mapinduzi ya kijeshihuwa na gharama.