1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaTunisia

Benki ya Dunia yasitisha uhusiano na Tunisia

Daniel Gakuba
7 Machi 2023

Benki ya Dunia imesema inaahirisha mazungumzo ya uhusiano wake wa baadaye na Tunisia, kufuatia kauli ya rais wa nchi hiyo, Kais Saied iliyochukuliwa kuwa ya chuki dhidi ya wahamiaji.

https://p.dw.com/p/4ON8Z
Australien-Währung - Australisches Geld
Picha: Rafael Ben-Ari/ Chameleons Eye/Newscom/picture alliance

Katika tangazo lilochapishwa na Benki ya Dunia Jumapili jioni, rais wa benki hiyo David Malpass alisema kuwa matamshi ya Rais Saied yamechochea unyanyasaji wenye misingi katika ubaguzi wa rangi, na kwamba taasisi hiyo imeahirisha mkutano kati yake na Tunisia hadi itakapotangazwa vinginevyo.

Hata hivyo, kulingana na taarifa ambazo zimethibitishwa na shirika la habari la AFP, Benki ya Dunia itaendelea kuihudumia miradi iliyopo tayari nchini Tunisia.

Mwezi uliopita Rais Kais Saeid alidai bila kutoa ushahidi, kwamba ilikuwepo njama ya kubadisha utambulisho wa Kiarabu wa watu wa Tunisia kupitia uhamiaji wa watu kutoka Afrika ya kusini mwa jangwa la Sahara.

Baada ya matamshi hayo, wahamiaji kutoka nchi za kiafrika walirudishwa nyumbani kuepuka ghasia dhidi yao.