1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Barabara muhimu zafunguliwa Kivu Kaskazini

2 Machi 2023

Gavana wa kijeshi mkoani Kivu Kaskazini mashariki mwa Kongo, Luteni jenerali constant Ndima ametangaza kufunguliwa kwa barabara zinazoelekea katika maeneo yote yanayozalisha kiwango kikubwa cha vyakula mkoani humo.

https://p.dw.com/p/4O9sd
DRC Goma Grenzzwischenfall
Picha: Alexis Huguet/AFP/Getty Images

Maeneo hayo ni pamoja na Masisi, Rutshuru  na maeneo  mengine yanayodhibitiwa na kundi la wapiganaji wa M23.

Kufunguliwa  tena kwa barabara hizo na vijiji vinavyo sambaza vyakula katika jiji hili, kumetangazwa wakati huu ambapo mamia ya malori yakubeba mizigo, yalianza kuwasili mjini jana jioni baada ya majuma kadhaa yakiwa yamezuiliwa na waasi wa M23 katika vijiji mbalimbali vinavyo shuhudia machafuko kwa zaidi ya mwezi moja sasa.

Hata hivyo, akiuhutubia mkutano wa wanahabari ,luteni kanali Guillaume Njike msemaji wake gavana wakijeshi ,amedai kuwa hii ni njia pekee ya kuwasaidia maelfu wa raia wanaohangaishwa na vita.

DRC Goma Grenzzwischenfall
Kivu Kaskazini ndilo eneo linalodaiwa kuzalisha chakula kwa wingi KongoPicha: Alexis Huguet/AFP/Getty Images

Raia wana hofu kuhusiana na ukosefu wa chakula

Wakati hatua hii  ya mamlaka yakijeshi imepongezwa na maafisa wa idara za usafiri jimboni humu, maafisa wa asasi za kiraia wameonekana kuwa na mashaka kufuatia mapigano na ukosefu wa usalama kwenye maeneo yalio tajwa  katika tangazo hilo .

Awali, raia wanao  ishi katika  vijiji wilayani Rutshuru  baadhi ikiwa ni wale wanao tegemea kilimo,walidai kuingiwa na hofu kufuatia ukosefu wa chakula unaotokana nakuzuiliwa kwao kutoelekea mashambani na kundi hilo la wapiganaji.

Hata hivyo wakaazi wa mji huu wa Goma waliotengwa  na mitaa inayozalisha chakula  kwa sababu ya vita,wamekuwa  pia na hisia tofauti .

Msururu wa magari yenye mizigo kutoka maeneo yanayoshikiliwa na waasi yameendelea kuingia mjini Goma nakushangiliwa na maelfu wa raia.