Bukele athibitishwa mshindi katika uchaguzi wa El Salvador
20 Februari 2024Matangazo
Hii ni baada ya zoezi jipya la kuhesabu kura kufanyika kwa mara nyingine.
Tume hiyo imesema kwamba takriban asilimia 30 ya masanduku ya kura yaliyotumiwa katika uchaguzi wa Urais na Bunge uliofanyika Februari 4, yalihesabiwa upya.
Rais wa El-Salvador ajitangaza mshindi wa uchaguzi
Rais Bukele amejipatia ushindi wa urais kwa asilimia 84 ya kura huku kukiwa kuliripotiwa hitilafu kadhaa katika mchakato wa kupakia data kwenye mfumo wa kielektroniki.