1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaUkraine

Zelensky atia saini makubaliano ya kiusalama na Ubelgiji

28 Mei 2024

Rais Volodymyr Zelensky wa Ukraine ametia saini Jumanne makubaliano ya kiusalama ya muda mrefu na Waziri Mkuu wa Ubelgiji Alexander De Croo mjini Brussels.

https://p.dw.com/p/4gN0M
Umoja wa Ulaya wamuunga mkono Zelensky katika vita vyake na Urusi
Umoja wa Ulaya wamuunga mkono Zelensky katika vita vyake na UrusiPicha: Jonas Roosens/ANP/IMAGO

Zelensky ametangaza makubaliano hayo ya dola bilioni 1.06 kupitia mtandao wake wa kijamii wa X.

Makubaliano hayo kando na mambo mengine yanaweka wazi ahadi ya Ubelgiji ya kuiunga mkono Ukraine katika muda wa miaka 10 ijayo.

Makubaliano hayo pia kwa mara ya kwanza yameeleza juu ya ndege 30 za kivita aina ya F-16 ambazo Ukraine itapokea, huku ndege ya kwanza ikitarajiwa kuwasili mwaka huu.

Makubaliano hayo ya usalama yametokea kufuatia uamuzi wa wakuu wa mataifa ya muungano wa NATO katika mkutano wa kilele uliofanyika mji mkuu wa Lithuania wa Vilnius mnamo mwezi Julai.

Wakati huo huo, mawaziri wa ulinzi wa Umoja wa Ulaya wanakutana mjini Brussels kujaribu tena kuondoa kiunzi cha Hungary cha kuzuia mpango wa kuipa Ukraine msaada mpya wa fedha.