1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroUkraine

Zelenskiy asifu juhudi za Saudi Arabia za kuwa mpatanishi

28 Februari 2024

Rais Volodymyr Zelenskiy amefanya mazungumzo nchini Saudi Arabia na mrithi wa kiti cha ufalme Mohammed bin Salman na kupongeza juhudi za utawala huo wa kifalme katika kutafuta suluhu ya mzozo kati ya Urusi na Ukraine.

https://p.dw.com/p/4cxiQ
Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskiy akiwasili katika Mkutano wa Wakuu wa Jumuiya ya Nchi za Kiarabu mjini Jeddah, Saudi Arabia.
Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskiy akiwasili katika Mkutano wa Wakuu wa Jumuiya ya Nchi za Kiarabu mjini Jeddah, Saudi Arabia.Picha: Saudi Press Agency/REUTERS

Taarifa kutoka ofisi ya Rais Volodymyr Zelenskiy imeeleza kuwa viongozi hao wawili wamejadili juu ya mpango wa amani wa kumaliza mzozo huo ambao umeingia mwaka wake wa tatu huku Zelenskiy akitoa shukrani kwa Mohammed bin Salman kwa jukumu lake la upatanishi.

Shirika la habari la serikali ya Saudi Arabia limeripoti kuwa, utawala huo wa kifalme umejitolea kimasomaso kuunga mkono juhudi zote za kimataifa zinazolenga kuutatua mzozo kati ya Urusi na Ukraine.

Soma pia: Urusi yaandaa mashambulizi mapya dhidi ya Ukraine 

Mohammed bin Salman amechukua jukumu muhimu kama mpatanishi wa mzozo huo, licha ya Saudi Arabia kuwa na uhusiano wa karibu na Urusi na kuunga mkono sera zake za nishati kupitia kundi la mataifa yanayozalisha mafuta kwa wingi duniani OPEC+.