1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

IOM: Zaidi ya watu milioni 7 ni wakimbizi wa ndani Sudan

Josephat Charo
6 Septemba 2023

Tangu kuzuka kwa vita nchini Sudan watu zaidi ya milioni saba wamekuwa wakimbizi wa ndani.

https://p.dw.com/p/4Vzca
Sudanesische Flüchtlinge, die vor dem Konflikt in Suda geflohen sind
Picha: Pierre Honnorat/WFP/AP/picture alliance

Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia uhamiaji IOM limesema watu takriban milioni 7.1 wamekuwa wakimbizi wa ndani nchini Sudan kutokana na vita vilivyoanza mnamo Aprili mwaka huu. Shirika hilo limesema zaidi ya asilimia 50 ni watu wapya waliolazimika kuyahama makazi yao kutokana na vita hivyo.

Shirika la IOM limesema sasa linatarajia watu milioni 1.8 kuikimbia Sudan kufikia mwisho wa mwaka huu na limetoa wito wa msaada wa dola bilioni moja kuwasaidia huku kukiwa na ripoti za ongezeko la kasi ya maambukizi ya magonjwa na vifo.