1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaChina

Xi Jinping ataka jeshi thabiti zaidi

13 Machi 2023

Rais wa China Xi Jinping, amesema anataka kuliimarisha jeshi la nchi yake na kulifanya kuwa kile alichokiita ‘Ukuta mkubwa wa chuma”.

https://p.dw.com/p/4Ob01
China | Volkskongress (NPC) in Peking
Picha: GREG BAKER/POOL/AFP/Getty Images

Amesema hayo kwenye hotuba yake ya siku ya mwisho ya kongamano la kila mwaka la Bunge la Wananchi. Amesema "Ni lazima tuendeleze kwa kikamilifu, uboreshaji wa ulinzi wa taifa, wa vikosi vyetu na  tujenge ukuta mkuu wa chuma, ambao unalinda kikamilifu uhuru wa taifa letu, usalama na masilahi yetu kimaendeleo.”

Bunge hilo liliidhinisha ongezeko la asilimia 7.2 kwenye bajeti kwa matumizi ya kijeshi, hiyo ikiwa ongezeko la juu kwa uwiano kuliko ongezeko lililopangwa la matumizi jumla.

Aidha alizungumzia pia mipango ya nchi yake ya kile alichokitaja kuwa ‘muungano' na Taiwan, japo alizungumza kwa sauti ya tahadhari.

Hakurudia kauli za awali kwamba China haitafutilia mbali uwezekano wa kutumia nguvu ya kijeshi kuhusu suala hilo.