Taarifa ya kufunga mwaka ya Jeshi la Polisi nchini Tanzania inaeleza kwamba idadi kubwa ya mauaji kwenye mwaka 2020 yalikuwa yanahusiana na sababu za wivu wa mapenzi ikilinganishwa na vile vya matukio mengine. Je, hii ina maana gani kwa maisha ya siku kwa siku ya Watanzania wa kawaida majumbani mwao? Msikilize Padri Leone Maziku, ambaye ni mtaalamu wa Saikolojia na Sosholojia kutoka Tanzania.