1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

WHO: Afrika ina barabara, gari chache lakini ajali nyingi

2 Oktoba 2024

Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya (WHO) linasema ingawa Afrika ina barabara na magari machache zaidi kuliko kanda nyingine, ndiyo yenye idadi kubwa kabisa ya vifo vya ajali za barabarani.

https://p.dw.com/p/4lKMs
Mojawapo ya ajali ya barabarani.
Mojawapo ya ajali ya barabarani.Picha: Oswaldo RivasAFP/Getty Images

Ripoti hiyo ya hivi karibuni ya WHO inasema ajali hizo zinachochewa na uzembe, mwendo mkali, ulevi, miundombinu mibovu na magari mabovu.  

Wataalamu wanasema maeneo mengine pia yanakabiliwa na changamoto kama hizo na nyingine kama za kutofunga mikanda ama kutovaa kofia ngumu.

Soma zaidi: Watu 32 wapoteza maisha ajali ya barabarani Misri

Lakini kwa Afrika, ambako vifo 620 vya barabarani hutokea kila siku, hali huwa ni mbaya zaidi kutokana na barabara mbaya, magari makuukuu na upungufu wa huduma za dharura. 

Ripoti hiyo ya WHO inasema Afrika imelitangulia eneo la kusini mashariki mwa Asia kwa kuwa na idadi kubwa zaidi ya vifo vya barabarani vya wastani wa watu 19.5 kati ya 100,000 kwa mwaka 2021.

Mwaka uliopita, Afrika - yenye asilimia 4 tu ya magari yote ulimwenguni - ilikabiliwa na asilimia 19 ya vifo vyote vya barabarani ulimwenguni.