1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Waziri wa Ulinzi wa Ujerumani ataka jeshi kujiandaa na vita

6 Juni 2024

Waziri wa Ulinzi wa Ujerumani Boris Pistorius jana Jumatano aliezea umuhimu wa kuliimarisha jeshi la Ujerumani, Bundeswehr, kujiandaa kwa vita kabla ya kumalizika kwa muongo huu.

https://p.dw.com/p/4ghtR
Jeshi la Ujerumani latakiwa kujiandaa kwa vita
Waziri wa Ulinzi wa Ujerumani ametaka jeshi la nchi hiyo kujirekebisha na kujiandaa kwa vita kabla ya kumalizika kwa muongo huuPicha: Thomas Koehler/photothek/picture alliance

Pistorius amesema jeshi la Ujerumani, Bundeswehr linatakiwa kuwa tayari kwa vita ifikapo mwaka 2029. Amesema hayo alipokuwa akijibu maswali ya wabunge jana Jumatano na kuongeza kuwa jeshi hilo linahitaji fedha zaidi, vifaa na wanajeshi watakaokuwa tayari kwa vita.

Amesema, katika hali ya dharura, wanahitaji wanaume na wanawake wenye nguvu watakoweza kulitetea taifa lao.

Pistorius aidha, amesema anadhani kuna sababu ya kuwa na mfumo mpya wa jeshi kama sehemu ya uimarishwaji huo, pamoja na kuiagiza wizara yake kutafuta watu wanaoweza kujiunga na jeshi.

Ujerumani ilisitisha mfumo wa kujiunga jeshini kwa hiyari mwaka 2011, lakini karibu nusu ya Wajerumani wanataka urejeshwe.