1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ujerumani kuisaidia Ukraine kukabiliana na vita vya Urusi

21 Juni 2023

Waziri wa mambo ya nje wa Ujerumani Annalena Baerbock ametangaza mipango ya nchi yake ya kuisadia Ukraine kukabiliana na vita vya Urusi, katika ufunguzi wa mkutano kuhusu kuijenga upya Ukraine, mjini London, Uingereza.

https://p.dw.com/p/4Stfr
Berlin | Aussenministerin Annalena Baerbock
Picha: Jens Krick/Flashpic/picture alliance

Baerbock ameahidi kwamba Ujerumani itatowa msaada kwa Ukraine katika kipindi cha mwaka huu, ambazo zitatumika kusimamia kwa mfano ununuzi wa  majenereta chakula na mahema.

Fedha sio hatua ya kutosha kuisaidia Ukraine

Hata hivyo waziri huyo wa Ujerumani ameongeza kusema kwamba fedha sio hatua ya kutosha kuisadia Ukraine na kwamba Ujerumani itasaidia nchi hiyo katika kuwekeza kwenye nishati mbadala na nishati ya uhakika.

Blinken atangaza msaada wa Marekani wa dola bilioni 1.3

Katika mkutano huo wa mjini London, awali pia waziri wa mambo ya nje wa Marekani Antony Blinken alitangaza msaada wa dola bilioni 1.3 utakaotolewa na nchi yake kwa ajili ya kuisadia ukraine ambapo milioni 520 zimekusudiwa kusaidia katika shughuli za ukarabati wa gridi ya nishati ya Ukraine.Uingereza inayoongoza mkutano huo kwa pamoja na Ukraine, imesema makampuni chungu nzima yametangaza kuwa tayari kuisadia Ukraine