1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Hossein Amir Abdollahian anaizuru Tanzania

25 Agosti 2022

Waziri wa mambo ya kigeni wa Iran Hossein Amir Abdollahian anaizuru Tanzania Alhamisi katika muendelezo wa ziara yake ya kwanza barani Afrika tangu alipoteuliwa kushika wadhifa huo. Mwanadiplomasia huyo tayari aliitembelea Mali tangu siku ya Jumatatu

https://p.dw.com/p/4G1HT

Ziara yake inafanyika katika wakati utawala wa rais mpya wa Iran Ibrahim Raisi unatafuta kuimarisha uhusiano zaidi na mataifa yanayoendelea. Lakini taifa kama Tanzania linanufaika vipi na mahusiano na Iran? Hilo ni miongoni mwa maswali ambayo Rashid Chilumba amemuuliza Mwenyekiti wa Kamati ya Mambo ya Nje ya Bunge la Tanzania, Vita Kawawa akiwa jijini Dar es Salaam.