1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kosovo: Genge la uhalifu lahusika shambulizi la Septemba

23 Oktoba 2023

Waziri mkuu wa Kosovo amedai kwamba genge la wahalifu kutoka kaskazini mwa Serbia lilihusika na shambulizi la mwezi Septemba lililosababisha kifo cha polisi mmoja na mapigano makali.

https://p.dw.com/p/4Xv2N
Waziri Mkuu wa Kosovo Albin Kurti
Waziri Mkuu wa Kosovo Albin KurtiPicha: DW

Waziri mkuu wa Kosovo amedai hii leo kwamba genge la wahalifu kutoka kaskazini mwa Serbia lilihusika na shambulizi la mwezi Septemba lililosababisha kifo cha polisi mmoja na mapigano makali yaliyodumu kwa siku nzima na polisi wa Kosovo, ambapo watu watatu waliuawa.

Waziri Mkuu Albin Kurti pia amedai kwamba Waziri wa Ulinzi wa Serbia Milos Vucecic ndiye anayeongoza kundi hilo linaloitwa Novi Sad Clan, na kuongeza kwamba Rais wa Serbia Aleksandar Vucic pia alikuwa na mahusiano na kundi hilo. Hata hivyo hakutoa ushahidi wa madai hayo. 

soma pia:Uingereza yatuma wanajeshi wake kulinda amani Kosovo

Wizara ya ulinzi ya Serbia imekana tuhuma hizo na kumtuhumu Kurti kwa kusema uongo, huku ikiiomba jamii ya kimataifa kuzuia kile ilichoita kampeni "chafu na za uchochezi" za uongozi wa Kosovo.  

Mapigano hayo yalirejesha wasiwasikati ya Kosovo na Serbia na yalikuwa mabaya kabisa kushuhudiwa tangu Kosovo ilipopata uhuru kutoka kwa Serbia 2008.