1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaAsia

Waziri mkuu mpya Pakistan aapishwa

14 Agosti 2023

Anwaar ul-Haq Kakar ameapishwa leo kuwa waziri mkuu wa mpito nchini Pakistan

https://p.dw.com/p/4V9Ba
Pakistan | Anwaar ul Haq Kakar wird neuer Interims-Premierminister
Picha: Senate of Pakistan/REUTERS

Anwaar ul-Haq Kakar ameapishwa leo kuwa waziri mkuu wa mpito nchini Pakistan atakayesimamia mchakato wa uchaguzi mkuu wakati nchi hiyo ikiwa inakabiliwa na mkwamo mkubwa wa kisiasa na kiuchumi. Kakar ameahidi kuilinda katiba ya nchi wakati akiapishwa na rais Arif Alvi katika sherehe iliyofanyika ofisi ya rais.Mwanasiasa huyo hana umaarufu mkubwa ingawa inaaminika yuko karibu na jeshi akitokea chama cha Awami cha Balochistan ambacho kinatazamwa kama chama kilichoko karibu zaidi na jeshi lenye usemi mkubwa katika maamuzi ya kitaifa.

 

DW Kiswahili | Saumu Mwasimba
Saumu Mwasimba Mhariri na mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya DW