MigogoroJamhuri ya Kidemokrasia ya Congo
Watu watano wauawa katika mlipuko wa bomu mashariki ya Kongo
20 Juni 2024Matangazo
Msemaji wa jeshi la Kongo katika eneo la Kivu Kaskazini Mak Hazukay amewalaumu waasi wa M23 kwa kuhusika na shambulio hilo. Hazukay amesema watu watatu wamejeruhiwa kwenye shambulio hilo.
Soma pia: AU walaani mauaji ya watu wengi nchini DR Congo
Kulingana na takwimu za Umoja wa Mataifa, vifo hivyo vinaonyesha hali mbaya inayowakabili wananchi kutokana na mgogoro wa zaidi ya miaka miwili kati ya majeshi ya Kongo na wanamgambo wa M23 wanaoungwa mkono na Rwanda.
Umoja wa Mataifa umesema takriban watu milioni 1.5 wamekiyambia makazi yao mashariki ya Kongo.