1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaIsrael

Watu 40 wauawa Israel katika mashambulizi ya Hamas

Daniel Gakuba
7 Oktoba 2023

Takriban watu 40 wameuwawa ndani ya Israel, katika shambulizi la kushtukiza lililofanywa na wanamgambo wa Kipalestina wa Hamas asubuhi ya leo.

https://p.dw.com/p/4XFK0
Jengo lililoshika moto baada ya mashambulizi Gaza
Jengo lililoshika moto baada ya mashambulizi GazaPicha: MAHMUD HAMS/AFP

Takwimu hizo zimetolewa na kitengo cha Israel cha magari ya kuwabeba wagonjwa ikisema kuwa idadi hiyo inajumuisha watu waliouawa kwa maroketi na katika hujuma za ardhini. 

Hamas imefyatua maroketi 2,200 kutokea Ukanda wa Gaza, katika kile ilichokitaja kuwa ni ''operesheni ya kijeshi.''

Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu amesema nchi yake iko vitani, na kuongeza kuwa maadui wa Israel ''watalipa gharama kubwa kwa kiwango ambacho hakijawahi kushuhudiwa''. 

Soma pia:Baada ya shambulio la Hamas, Netanyahu asema Israel iko vitani

Pande mbali mbali duniani, zikiwemo Marekani, Umoja wa Ulaya na jumuiya ya kujihami ya NATO zimelaani mashambulizi hayo ya Hamas, na kuelezea mshikamano na Israel na watu wake. 

Rais wa Mamlaka ya Wapalestina Mahmoud Abbas amesema Wapalestina wanayo haki na kujilinda, huku Saudi Arabia na Misri zikizitaka pande zote kuwa na ustahimilivu.

Wakati huohuo, wizara ya afya ya Gaza imesema kuwakaribu watu 200 wameuwawa baada ya mashambulizi yaliyofanywa na jeshi la Israeli  katika ukanda huo kama hatua ya kujibu mashambulizi. Watu wengine 1600, wamejeruhiwa katika tukio hilo.