1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaAsia

Watu 45,000 wakimbia makaazi yao Rakhine

24 Mei 2024

Umoja wa Mataifa unasema kwamba mapigano yanayoongezeka katika jimbo linalozongwa na machafuko la Rakhine nchini Myanmar yamewalazimisha takribani watu 45,000 kuyakimbia makaazi yao.

https://p.dw.com/p/4gEew
Myanmar | gwaride la jeshi
Jeshi la Myanmar kwenye gwaride katika mji mkuu, Naypyidaw.Picha: Aung Shine Oo/AP Photo/picture alliance

Umoja wa Mataifa ulisema siku ya Ijumaa (Mei 24) kwamba wengi wa waathiriwa wanatoka jamii ya Waislamu wa Rohingya, huku kukiwa na madai ya watu kuuawa na mali kuchomwa moto.

Soma zaidi: Guterres "asikitishwa" na mauwaji Myanmar

Akizungumza na waandishi habari mjini Geneva, msemaji wa Shirika la Haki za Binaadamu la Umoja wa Mataifa, Elizabeth Throssell, alisema katika siku za hivi karibuni, makumi kwa maelfu ya raia wameyakimbia mapigano yanayoendelea katika viunga vya Buthidaung na Maungdaw.

Soma zaidi: UN yasikitishwa na mashambulizi ya anga yanayoendelea Myanmar

Throssell alisema kuwa Warohingya wanaokadiriwa kuwa 45,000 wameripotiwa kukimbilia eneo la Mto Naf karibu na mpaka wa Myanmar na Bangladesh wakitafuta usalama.