1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
JamiiBrazil

Watu 36 wafariki kutokana na mafuriko Brazil

20 Februari 2023

Watu wapatao 36 wamekufa baada ya mvua kubwa kusababisha mafuriko na maporomoko ya udongo katika jimbo la Sao Paulo nchini Brazil.

https://p.dw.com/p/4Njj9
Brasilien Unwetter l Zerstörung nach heftigem Regen in Sao Sebastiao
Picha: Sao Sebastiao City Hall /AFP

Maafisa wamesema watu 35 wamekufa katika mji wa Sao Sebastiao kusini mashariki mwa Brazil, na mmoja amekufa katika mji wa Ubatuba.

Wafanyakazi wa uokozi wakisaidiwa na helikopta, walikuwa wanawatafuta waathirika zaidi. Kwa mujibu wa taarifa za vyombo vya habari, watoto ni miongoni mwa watu waliokufa.

Gavana wa Sao Paulo, Tarcisio de Freitas, ametangaza hali ya hatari kwenye manispaa tano zilizoathiriwa.

Rais wa Brazil, Luiz Inacio Lula da Silva, leo anatarajiwa kulizuru eneo hilo. Makaazi ya zaidi ya watu 330 yameharibiwa na barabara kadhaa zimefungwa kutokana na mvua hizo zilizoanza kunyesha siku ya Jumamosi.