1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Watanzania sasa kula nyamapori bila kificho

Prosper Kwigize15 Aprili 2021

Tanzania imeanza utekelezaji wa mpango wa uvunaji endelevu wa wanyamapori kwa kuanzisha maduka ya nyama za porini kwa ajili ya wananchi. Utekelezaji huo ambao ni sehemu ya maagizo ya alitekuwa Rais wa Tanzania hayati Dr. John Pombe Magufuli umeanza Jumatano wilayani Mpanda mkoani Katavi kwa kufungua duka la kwanza la nyama zinazotokana na wanyamapori.

https://p.dw.com/p/3s3qB

Wakati kukiwepo malalamiko ya wananchi kutofaidi rasilimali za taifa hususani wanyamapori, jambo linalochochea kuwepo kwa uwindaji haramu, watanzania sasa wataanza kunufaika na kitoweo cha wanyamapori bila kificho. 

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo meneja wa Lengo la mradi huo Mwakilishi wa mamlaka ya wanyamapori Tanzania ambaye pia ni meneja wa porii la akiba Rukwa Bw. Goodluck Baragaye amebainisha kuwa lengo ni kudhibiti ujangiri pamoja na kuhamasisha jamii kushiriki uhifadhi.

Hata hivyo kumekuwepo mashaka ya uendelevu wa biashara hiyo, kutokana na hofu hiyo Mkuu wa mkoa wa Katavi Bw. Juma Homera amesema kutokana na idadi ya Wanyama waliopo sambamba na ukubwa wa misitu ya hifadhi, maduka hayo ya nyama yatakuwa endelevu.

Hii ni mara ya kwanza kwa Tanzania kanzisha huduma ya uuzaji wa kitoweo cha wanyamapori, licha ya kwamba zilikuwa zikiuzwa katika hoteli kubwa jijini Dar es salaam na Arusha ambapo wananchi wa kawaida hawakuwa na fursa ya kununua.