1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

watalii tisaa wa kijerumani wamefariki dunia kufuatia ajali katika milima ya Alp ya Austria

6 Septemba 2005
https://p.dw.com/p/CEe5

Berlin:

Watalii wa kijerumani wasiopungua tisaa wamekufa katika ajali ya chombo cha usafiri katika milima ya Alp nchini Austria.Chanzo cha ajali hiyo ni contena lililodondoka toka ndani ya helikopta moja huko Sölden-Tirol.Chombo kimoja cha usafiri wa milimani kilianguka na vyengine viwili vikaanza kubiringika na kuwandondosha waatu waliokuwemo ndani yake.Shirika la msalaba mwekundu limesema watu wengi wamejeruhiwa vibaya sana.Zaidi ya abiria mia moja walibidi kuokolewa.