1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaSudan

Wanamgambo wa RSF waonesha dhamira ya kusitisha mapigano

3 Januari 2024

Kikosi cha wanamgambo wa RSF nchini Sudan kimeonyesha utayari wake wa kusitisha mara moja mapigano na bila masharti yoyote kupitia mchakato wa mazungumzo na Jeshi la Sudan.

https://p.dw.com/p/4aoyN
Sudan 2019 | Mwanajeshi wa kikosi cha RSF
Mapigano kati ya RSF na jeshi la Sudan limeitumbukiza nchi hiyo kwenye mzozo mkubwa tangu Aprili mwaka 2023.Picha: Hussein Malla/AP Photo/picture alliance

RSF imetia pia saini tamko na muungano wa kiraia "Taqadum" na kulitaka pia jeshi kufanya hivyo.

Vita vya miezi tisa nchini Sudan, ambayo sasa inakabiliwa na mzozo mkubwa zaidi duniani wa watu walioyahama makazi yao, umeharibu miundombinu ya nchi hiyo na kuzusha tahadhari za kutokea baa la njaa.

Majaribio ya kumaliza mzozo huo kwa njia ya mazungumzo yakiongozwa na Marekani na Saudi Arabia, hadi sasa yameambulia patupu huku makubaliano ya awali ya kuwalinda raia yakipuuzwa.

Kwa kutia saini kile kinachoitwa "Azimio la Addis Ababa" ambalo linakusudiwa kutumika kama msingi wa kufanyika mazungumzo zaidi na suluhisho la kisiasa, RSF imeonyesha nia ya wazi ya kuvimaliza vita hivyo.